Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dkt.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Dini, Wanafamilia na Wananchi katika Sala ya Maiti ikiongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, kumsalia Marehemu Hafidh Ameir Hassan Mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, iliyofanyika katika Msikiti wa Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja leo 7-9-2026.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa heshima za mwisho kwa Marehemu Hafidh Ameir Hassan, mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika mazishi yaliyofanyika leo, tarehe 07 Septemba 2026, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa, Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, viongozi wa dini, pamoja na familia, ndugu, jamaa na wananchi mbalimbali.
Mapema, Rais Dkt. Mwinyi ameungana na familia, ndugu na jamaa katika Sala ya Jeneza iliyofanyika Masjid Ihtiswam, Kizimkazi, kabla ya mwili wa Marehemu Hafidh Ameir Hassan kuzikwa katika makaburi maalum ya Kizimkazi.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ametoa mkono wa pole kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, watoto na familia ya Marehemu, na kuwafariji katika kipindi hiki cha majonzi.
Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Raji’un.











0 Comments