6/recent/ticker-posts

MHE. BALOZI OMAR: SEKTA BINAFSI NI INJINI YA TANZANIA KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kushoto), akishiriki mjadala ukiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt), Bw. David Tarimo, katika halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine alitoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Na. Peter Haule na Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam

Serikali imetoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati alipokuwa Mgeni Rasmi katika halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam.

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wenye thamani ya takribani dola za Marekani trilioni moja, huku pato la mtu mmoja mmoja likitarajiwa kuvuka dola 7,000 ifikapo mwaka 2050, lakini pia uchumi wa viwanda, jumuishi na unaoongozwa na sekta binafsi.

“Utekelezaji wa Dira 2050 kupitia Mpango wa Muda Mrefu wa Maendeleo na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano (FYDP IV) umeweka msisitizo mkubwa kwa sekta binafsi, ambapo mfumo wa uwekezaji wa uwiano wa asilimia 70 kwa 30 unaiweka sekta binafsi kama injini kuu ya ukuaji na ufadhili wa maendeleo” alisema
Mhe. Balozi Omar

Aliongeza kuwa Utekelezaji wa FYDP IV unahitaji uwekezaji unaokadiriwa kufikia takribani Shilingi trilioni 477, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kugharamia takribani asilimia 70, sawa na Shilingi trilioni 324.49.

Mhe. Balozi Omar, alisisitiza kuwa takwimu hizo zinaonesha wazi kuwa Tanzania haiwezi kufikia malengo yake ya maendeleo kwa kutegemea bajeti ya Serikali, mikopo ya nje au misaada ya maendeleo pekee, bali inapaswa kuongeza uwezo wa kukusanya na kutumia mitaji ya ndani na ya sekta binafsi.

Akizungumzia Mfumo wa fedha, Mhe. Balozi Omar alisema sekta ya fedha nchini imeendelea kuwa imara licha ya changamoto na misukosuko ya uchumi duniani, ikiwa imechangiwa na misingi imara ya uchumi na shughuli endelevu za kiuchumi na mageuzi mbalimbali katika sekta hiyo yameendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ukuaji wa sekta huku mikopo kwa sekta binafsi ikikua kwa wastani wa zaidi ya asilimia 20 na mikopo chechefu ikiendelea kudhibitiwa chini ya kiwango kinachopendekezwa cha asilimia tano.

“Mchango wa sekta ya fedha katika Pato la Taifa umeongezeka hadi kufikia asilimia 4.3, huku ujumuishaji wa kifedha kwa watu wazima ukifikia asilimia 76, Maendeleo haya yanatoa msingi mzuri wa kuongeza uwezo wa mfumo wa fedha katika kukusanya akiba na kuzielekeza kwenye uwekezaji wenye tija” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aidha, alisema Serikali inakamilisha mchakato wa kuidhinisha awamu ya pili ya Blueprint for Regulatory Reforms (MKUMBI II), ambayo inalenga kuendana na mabadiliko ya sasa ya kiuchumi, kiteknolojia na kibiashara sambamba na kuendelea kufanya mageuzi ya kisheria, kiutawala na kitaasisi yanayolenga kurahisisha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.

Alisisitiza umuhimu wa kuongeza uwekezaji wa ndani, akieleza kuwa pamoja na uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDI) umeongezeka kutoka dola milioni 1,656 mwaka 2024 hadi dola milioni 1,718 mwaka 2025, sawa na ongezeko la asilimia 3.7, kuwa muhimu katika kuleta mitaji, teknolojia, utaalamu na masoko ya kimataifa, Watanzania wanapaswa kuwezeshwa kushiriki zaidi katika kuwekeza ndani ya uchumi wao wenyewe.

“Nawasisitiza umuhimu wa kuimarisha na kuongeza ushiriki katika masoko ya mitaji nchini, akieleza kuwa masoko yenye kina na ukwasi yanaweza kuwa chanzo muhimu cha mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya uwekezaji na Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kisheria na udhibiti yatakayowezesha kuibuka kwa bidhaa mbalimbali za masoko ya mitaji, huku ushiriki wa wananchi katika hati fungani za Serikali, mifuko ya uwekezaji na soko la hisa ukiendelea kuhamasishwa” alisema Mhe. Balozi Omar.

Aliongeza kuwa Tanzania tayari ina msingi mzuri wa kifedha unaojumuisha mfumo wa benki unaokua, mifuko ya pensheni na taasisi za fedha zenye mali zinazoongezeka, ushiriki mkubwa wa wananchi katika bidhaa rasmi za uwekezaji, masoko ya mitaji yanayopanuka pamoja na sekta binafsi yenye nguvu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt), Bw. David Tarimo, alisema mjadala huo umejikita katika namna ya kubadilisha akiba zilizopo nchini kuwa mtaji wa kukuza uchumi na kuongeza upatikanaji wa mtaji wa ndani.

Alisema mjadala huo pia umeangazia malengo makubwa yaliyowekwa kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka 50, ambayo kwa kiasi kikubwa yanategemea ushiriki na uwekezaji wa sekta binafsi, na Mpango wa Tano wa Maendeleo wa Miaka Mitano umeweka msisitizo mkubwa zaidi katika uwekezaji wa sekta binafsi ikilinganishwa na mipango ya miaka iliyopita.

Bw. Tarimo amesema kikao hicho kimewapa wadau fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kuimarisha mazingira ya uwekezaji na kuongeza uwezo wa sekta binafsi kushiriki kikamilifu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa.

“Jukwaa hili lmepata fursa ya kusikiliza mipango ya Serikali kuhusu utekelezaji wa Dira hiyo, huku wajumbe nao wakitoa mawazo na mapendekezo yanayolenga kusaidia kufanikisha malengo hayo” alisema Bw. Tarimo

Aliongeza kuwa CEOrt itaendelea kushirikiana na Serikali kubaini maeneo yanayohitaji maboresho na kuunga mkono mageuzi katika kanuni na taratibu, ili kujenga mazingira ya biashara yaliyo rafiki, rahisi na yenye gharama nafuu, hususan kwa wafanyabiashara wadogo.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo pa moja na mambo mengine alitoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.
Baadhi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt), wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani) aliyekuwa Mgeni rasmi katika halfa ya Mjadala wa Bodi ya Wakurugenzi na Wajumbe wa Jukwaa la Wakurugenzi Wakuu wa Tanzania (CEOrt) unaofanyika kila Mwezi” Board of Directors and Members of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt) Monthly Dialogue”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine alitoa wito kwa wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na sekta binafsi nchini kuunganisha nguvu katika kubadili akiba za Watanzania kuwa mitaji ya uwekezaji yenye tija, itakayochochea uzalishaji, kuongeza ajira, mauzo ya nje na kukuza uchumi kwa mujibu wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)


Post a Comment

0 Comments