Na Rahma Khamis
Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Bi Daulat Abdallah Said amewataka wahitimu waliomaliza mafunzo ya mbinu za kufindishia kiswahili kwa wageni kushirikiana kwa pamoja ili kuendeleza ujunzi waliyopatiwa katika kipindi chote cha mafunzo hayo
Akifunga mafunzo ya siku Tano katika Ukumbi wa Nyumba ya Sanaa Mwanakwerekwe, amesema licha ya kuhitimu mafunzo hayo lakini bado wana nafasi ya kujiendeleza kwa kutafuta vitabu mbalimbali kwa ajili ya kujisomea na kukuza vipaji vyao
Amesema kuwa walimu wa kiswahili wana jukumu la kuwafundisha wageni lugha hiyo sambamba na kufundisha Utamaduni wa kizanzibar ili kuifahamu
Kaimu amefahamisha kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuitumia fursa ya kiswahili ndani na nje ya nchi kwa kujiajiri na kujipatia kipato
Aidha amewataka wahitimu hao kutumia lugha hiyo owa fasaha na Sanifu kwa wageni ili kuifahamu kwa wepesi wakati wa kujifunza
" tuna jukumu la kufundisha wageni Utamaduni weti ili kufahamu taratibu zetu hasa katika maamkizi" alisema Kaimu
Nae Mratibu wa mafunzo kutoka BAKIZA Zakia Mustafa Fatawi amewahimiza wahitimu wa Mafunzo hayo kuyafanyia kazi kushirikiana na kufanya bidii ya kujiendeleza kielimu ili kufikia malengo
Akizungumza kwa niaba ya wenzake mhitimu bi Fatma Hamza Amir amelishukiru Baraza la kiswahili kwa kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yatawasaidia kupata faida hapo baadae




0 Comments