6/recent/ticker-posts

Wahitimu wa Mafunzo ya Kiswahili Watakiwa Kutumia Mbinu za Kufundishia Kiswahili Kwa Wageni

Na Rahma Khamis

Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Bi Daulat Abdallah Said amewataka wahitimu waliomaliza mafunzo ya mbinu za kufindishia kiswahili  kwa wageni kushirikiana kwa pamoja ili kuendeleza ujunzi waliyopatiwa katika kipindi chote cha mafunzo hayo

Akifunga mafunzo ya siku Tano katika Ukumbi wa Nyumba ya Sanaa Mwanakwerekwe, amesema licha ya kuhitimu mafunzo hayo lakini bado wana nafasi ya kujiendeleza kwa kutafuta vitabu mbalimbali kwa ajili ya kujisomea na kukuza vipaji vyao

Amesema kuwa walimu wa kiswahili wana jukumu la kuwafundisha wageni lugha hiyo sambamba na kufundisha Utamaduni wa kizanzibar ili kuifahamu

Kaimu amefahamisha kuwa lengo la  mafunzo hayo  ni kuitumia fursa ya kiswahili ndani na nje ya nchi kwa kujiajiri na kujipatia kipato

 Aidha amewataka wahitimu hao kutumia lugha hiyo owa fasaha na Sanifu  kwa wageni ili kuifahamu  kwa wepesi wakati wa kujifunza

" tuna jukumu la kufundisha wageni Utamaduni weti ili kufahamu taratibu zetu  hasa katika maamkizi" alisema Kaimu

Nae Mratibu wa mafunzo kutoka BAKIZA Zakia  Mustafa Fatawi amewahimiza wahitimu wa Mafunzo hayo kuyafanyia kazi kushirikiana na kufanya bidii ya kujiendeleza kielimu ili kufikia malengo

Akizungumza kwa niaba ya wenzake mhitimu bi Fatma Hamza Amir  amelishukiru Baraza la kiswahili kwa kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yatawasaidia kupata faida hapo baadae

Mafunzo hayoi wameshikisha wahitimu 35 ambapo wamekabidhiwa vyeti na kupata nafasi ya kufanya mazoezi kwa vitendo.

Post a Comment

0 Comments