Kamishna wa Polisi Zanzibar CP. Kombo Khamis Kombo amekutana na Wakuu wa Polisi wa Wilaya za Zanzibar na kuwataka kuwajibika katika kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu ili kupunguza uhalifu katika Visiwa vya Zanzibar.
Akizungumza na Wakuu hao wa Polisi Wilaya leo Agosti 26,2026 huko Makao Makuu ya Polisi Kamisheni ya Zanzibar amesema Viongozi hao wana jukumu la kusimamia Askari kufanya kazi kwa weledi katika kupunguza makosa ya jinai na makossa ya usalama barabarani na kuhakikisha maeneo yao yanakuwa salama.
Nae Naibu Mkurugenzi wa Upelezi wa Makosa ya Jinai, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) ZUBERI CHEMBERA amewahimiza wakuu wa Polisi Wilaya kuongeza nguvu katika kuzuwia uhalifu wanaofanyiwa watalii ili wageni wanaokuja kutalii Zanzibar wabaki salama.
Kitengo cha Habari
Makao Makuu ya Polisi
Zanzibar
0 Comments