Mke wa Rais wa Zanzibar , Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mama Mariam Mwinyi, akizungumza na Wanawake wajawazito na waliojifungua hivi karibuni, wakati alivyotembelea Taasisi ya Taasisi ya WAJAMAMA Zanzibar, Mbweni, Mkoa wa Mjini Magharibi tarehe 31 Agosti 2026.
Mke wa Rais wa Zanzibar , Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mama Mariam Mwinyi, ametoa wito wa kuimarishwa kwa huduma za afya ya mama na mtoto, elimu ya afya pamoja na lishe bora, akisema hatua hizo ni muhimu katika kupunguza vifo na kujenga jamii yenye afya na ustawi.Mama Mariam Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 31 Agosti 2026, wakati alipotembelea Taasisi ya WAJAMAMA Zanzibar, Mbweni, Mkoa wa Mjini Magharibi leo tarehe 31 Agosti, 2026 ambapo ameipongeza kwa juhudi za kutoa elimu na huduma zinazolenga kuboresha afya ya wanawake, wajawazito na watoto..jpg)






0 Comments