6/recent/ticker-posts

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla Amefungua Tawi la TIRA -- Chake chake Pemba

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Afisi za Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) Kanda ya Pemba zilizopo katika Jengo la Shirika la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) Madungu Chake - Chake Pemba. 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema Sekta ya Bima ni nguzo muhimu katika kukuza kipato cha mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo katika hafla ya uzinduzi wa Afisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania ( TIRA ) Kanda ya Pemba.

Amesema uziduzi wa Afisi ya TIRA Kisiwani Pemba utarahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo elimu kuhusu bima, usimamizi wa shughuli za bima, utatuzi wa changamoto zinazowakumba watumiaji wa bima pamoja na kuimarisha ufuatiliaji na utekelezaji wa sheria pamoja na kanuni za sekta za bima.

Mhe. Hemed amefahamisha kuwa kadiri uchumi unavyozidi kukua na umuhimu wa bima ndivyo unavyozidi kuongezeka katika kujenga ustahmilivu wa wananchi na taasisis dhidi ya majanga na hatari mbali mbali hivyo amewataka wananchi kufahamu kuwa  huduma za bima sio anasa bali ni nyenzo muhimu ya kulinda maisha, mali, uwekezaji, na shughuli za uzalishaji.

Makamu wa pili wa rais wa Zanzibar  ameielekeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania kuandaa utaratibu wa kutoa elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari, taasisi za elimu, vikundi vya kijamii na viongozi wa dini ili kuongeza uelewa wa wananchi juu ya umuhimu wa matumizi ya huduma ya bima.

Sambamba na hayo Mhe. Hemed  amewataka TIRA kukuza matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma na kushirikiana kwa karibu na taasisi za kifedha na wadau wengine ili sekata ya bima izidi kukua na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi.

Aidha, Mhe. Hemed amewafahamisha wananchi kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mbamo mnamo mwaka 2023 zimepitisha Sheria ya Afya kwa upande wa Tanzania Bara na Sheria ya kuanzishwa Mfuko wa huduma za Afya kwa Zanzibar kwa shabaha ya kuhakikisha kila kila mwananchi wa Tanzania anapata huduma bira za matibabu hata kama hana uwezo wa kulipia huduma za matibabu.

Hata hivyo amezitaka Taasisi za Umma na Sekta binafsi, madereva na wananchi wote wenye vyombo vya usafiri kuhakikisha wanavikatia biama kwa mujibu wa Sheria na kuzielekeza Mamlaka zinazosimamia usalama barabarani kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria na kuchukua hatua stahiki kwa wale wote wanaovunja Sheria za usalama barabarani.

Nae Naibu Waziri Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Dkt. Hamah Omar Bakar amesema uwepo wa Ofisi za TIRA Kisiwani Pemba zitaimairisha na kufikisha huduma za bima karibu na jamii, wafanyabiashara na wawekezaji kama nyenzo muhimu katika kulinda maisha ya watu, mali na shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Dkt. Hamad amefahamisha kwamba Ofisi hio itasaidia  kutatua changamoto na migogoro itokanayo na Bima ili kuhakikisha Sekta ya Bima inaendelea kuwa salama na kutanua wigo mpana katika kuwahudumia wananchi.

Kwa upande wake Kamishna mkuu wa Bima Tanzania ndugu Baghayo Saqware amesema Uzinduzi wa Afisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Kisiwani Pemba ni utekelezaji wa maagizo ya Serikali ya kufikisha huduma za bima karibu na wananchi ili waweze kupata huduma hizo kwa wakati, uhakika na ubora unaohitajika. 

Saqware amesema TIRA imekuwa ikofanya kazi ya  kifikisha elimu ya Bima kwa wananchi, utatuzi wa changamoto na migogoro inayotokana na Bima pamoja na kusimamia sekta ya Bima kwa uwazi, Ubunifu na kuzingatia matumizi ya Teknolojia ili huduma za Bima ziweze kumfikia mwananchi popote alipo Tanzania.

Aidha, Saqware amefahamisha kuwa kutokana na utayari wa watendaji na wadau mbali mbali wa kufanya kazi kwa kushirikia wameiwezesha TIRA kupata  mafanikio  makubwa  ikiwemo kuchangia katika ukuwaji wa uchumi wa Taifa (GDP) kwa aslimia 2.11 kwa mwaka 2025,  kuongezeka kwa gawio la TIRA Serikalini na kufikia Bilioni 5.13 mwaka 2025  pamoja na kutanua wigo wa mtandao wa Ofisi za TIRA hadi kufikia ofisi 13 mwaka 2025.

Nao wananchi wa Pemba wameipongeza Mamla ya Usimamizi wa Bima Tanzaia (TIRA) kwa kuona umuhimu wa kufungua Ofisi yao kisiwani Pemba jambo litakalo saidia kupatikana kwa huduma za bima kwa urahisi na usalama zaidi.

Wameimba TIRA kwa kuhakikisha wanatoa elimu zaidi kuhusu umuhimu wa bima kwa watu na mali zao ili waweze kukata bima na kujikinga na majanga mbali mbali yanayotokea bila  ya kutarajiwa.



Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR )

Leo..... Ogast 7, 2026.

Post a Comment

0 Comments