Sekta binafsi nchini inatarajiwa kuchangia takribani asilimia 70 ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Ujumbe wa GCF ulifanya ziara yake nchini Tanzania kuanzia Agosti 11 hadi 14, 2026 na Wadau mbalimbali nchini wa eneo la Fedha za Mabadiliko ya tabianchi mkoani Simiyu na Jijini Dar es Salaam.
Miongoni mwa nguzo tatu zinazounda Dira 2025 ni pamoja na Uchumi Imara, Jumuishi na Shindani ambayo inafungua fursa za kiuchumi na hivyo kuweka mazingira ya kupunguza umaskini na kuboresha hali ya maisha ya wananchi wote.
Aidha, Nguzo ya pili ni Uwezo wa Watu na Maendeleo ya Jamii ambayo inalenga kuimarisha uwezo wa watu na ustawi wa jamii, ikiwa na dhamira ya dhati katika kuleta usawa wa kijinsia kwa wote na kuwa na jamii jumuishi. Ili kutumia mbinu thabiti zikiambatana na kudumisha maadili mema, kujenga hulka ya kujiamini na kujifunza bila ukomo.
Uchumi imara utahakikisha kwamba maendeleo ya kiuchumi yanawanufaisha wananchi wote na hivyo katika muktadha huu, Tanzania imeendelea kupiga hatua za kiuchumi na kukua kwa wastani wa asilimia 6.2 kwa mwaka katika kipindi cha miongo miwili iliyopita.
Yote hayo yanawezakana kupitia usimamizi endelevu wa mazingira ambao umetajwa pia kama Nguzo ya tatu ambayo ni Uhifadhi wa Mazingira na Ustahimilivu wa Mabadiliko ya Tabianchi.

0 Comments