6/recent/ticker-posts

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla Amefunzu Maonesho ya Nane Nane Dole

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akivua pili pili boga katika shamba wakati akitembelea maonesho ya nane nane yanayoendeea katika viwanja vya maonesho Dole wilaya ya magharibi “ A “ Unguja.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema  Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanaendelea kuwa jukwaa muhimu la kuonesha mafanikio ya Sekta ya kilimo na mchango wa wakulima.

Ameyasema hayo kwa niaba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi katika hafla ya ufunguzi wa maonesho ya kumi (10) ya Kilimo Nane Nane yanayofanyika Dole  Kizimbani Wilaya ya Magharibi "A" Unguja. 

Amesema Maonesho ya Kilimo ya Nane Nane ni fursa kwa wakulima na wafugaji kubadilishana uzoefu, kukuza biashara na uwekezaji pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, Sekta binafsi, Washirika wa maendeleo na wannachi wote kwa ujumla. 

Mhe. Hemed amesema ili wananchi waendelee kushiriki kwa wingi katika maonesho hayo ubinifu zaidi unahitajika pamoja na kutoa elimu kwa wakulima ili waweze kuondokana na kilimo cha kujikimu na kwenda katika kilimo endelevu cha biashara kinachostahamili mabadiliko ya hali ya hewa na kuongeza thamani kwa utoshelevu wa chakula na mauzo ya ndani na nje. 

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar amesema kwa sasa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo imepata mafanikio makubwa ikiwemo kukamilika kwa mfumo wa Kilimo App, kukuza usajili wa wakulima, kukamilika kwa Maabara Mpya ya Utafiti wa Magonjwa ya Mifugo Kizimbani na kukamilika kwa Kituo cha masoko ya mazao ya nyuki Chamanangwe Pemba. 

Mhe. Hemed amefahamisha kuwa Serikali itaendelea kuekeza katika kilimo cha umwagiliaji, mbegu bora, mifugo, pembejeo, tafiti za kilimo na matumizi ya Teknolojia ili kuongeza uzalishaji na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. 

Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesisitiza kuwa ili kufikia maendeleo endelevu ya Sekta ya kilimo ni lazima kuwawezesha vijana na wanawake kwa kiwajengea uwezo kama vile kuwapatia ujuzi, mitaji, teknolojia ya kisasa na masoko jambo litakaloleta ustawi wa wakulima na wafugaji na kukua zaidi kwa sekta ya kilimo. 

Nae Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Mhe. Suleiman Masoud Makame amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kuekeza zaidi katika kilimo ili  kuhakikisha Zanzibar inajitosheleza kwa chakula na kuacha kuagiza chakula kutoka nje ya Zanzibar. 

Amesema ili kufikia malengo hayo Wizara ya kilimo kwa kushirikiana na wadau na washirika mbali mbali wa maendeleo imejipanga kufikisha elimu, ujuzi na nyenzo za kisasa kwa wakulima na wafugaji ili kutanua wigo mpana katika Sekta ya Kilimo na Ufugaji. 

Kwa upande wake Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Tanzania Mhe. Mwasi Damas Kamali ameipongeza wizara ya Kilimo Zanzibar kwa kupiga hatua katika maonesho ya Kilimo ya Nane Nane kwa kuweza kuziweka pamoja sekta za kilimo, Mifugo, uvuvi, maliasili na kuwarahisishia wananchi kuweza kujifunza na kupata bidhaa mbali mbali kwa urahisi kupitia maonesho hayo. 

Mhe. Mwasi amesema vijana na wanawake wamehamasika kushiriki kwa wingi katika shughuli za kilimo na ufugaji hivyo ipo haja kupewa kipaombele katika kuwawezesha ili waweze kufikia malengo yao. 

Mapema  Katibu Mkuu wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo ndugu Saleh Mohamed Juma amesema katika maonesho  ya Mwaka 2026 Wizara imefanikiwa kuboresha miundombinu na kuweka mazingira mazuri zaidi katika viwanja vya Maonesho Dole ambapo Jumla ya shilingi Milioni 750 zimetumika katika uboreshaji huo. 

Amesema kila mwaka maonesho hayo yamekuwa kuimarika na kuongezeka idadi ya washiriki ambapo kwa mwaka huu jumla ya washiriki 498 kutoka Zanzibar, Tanzania Bara na nje ya Tanzania wameshiki katika maonesho hayo jambo linalodhihirisha utayari wa wananchi hususan vijana na wanawake kujishughulisha na shughuli za kilimo na ufugaji. 

Saleh amewashauri wananchi kutembelea mabanda ya maonesho ili kupata elimu ya kilimo na ufugaji itakayowawezesha kulima kilimo cha kisasa na kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua. 

Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. alikagua na kuonea shunguli mbali mbali zinazofanywa na wakulima na wafugaji pamoja na kupokea maandamano ya magari yanayoweza kulima kisasa.

 

Imetolewa na kitengo cha habari ( OMPR )

Leo tarehe…..08 / 08 / 2026

Post a Comment

0 Comments