Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akisalimia na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Évariste Ndayishimiye, aliyeambatana na Mkewe, Mhe. Angeline Ndayishimiye, alipowasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Zanzibar leo tarehe 09 Septemba 2026, Ikulu Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Évariste Ndayishimiye, aliyeambatana na Mkewe, Mhe. Angeline Ndayishimiye, pamoja na ujumbe wake, leo tarehe 09 Septemba 2026, Ikulu Zanzibar.
Rais Ndayishimiye aliwasili Zanzibar jana, tarehe 08 Septemba 2026, kwa ajili ya kutoa salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Hafidh Ameir Hassan, na kuungana na familia katika kipindi hiki cha maombolezo.


0 Comments