Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Ndg. Abdi Mahamoud Abdi, amewataka watu wote waliojimilikisha maeneo na mali za chama hicho kinyume na taratibu kuzirejesha mara moja, kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.
Amesema hayo wakati wa ziara yake ya kwanza ya kukagua mali, maeneo na vitegauchumi vinavyomilikiw
a na CCM katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kusini Pemba, ikiwemo Wilaya za Mkoani na Chake Chake.
Amesema chama kinamiliki maeneo ya kimkakati ambayo yakisimamiwa na kutumika ipasavyo yanaweza kuwa chanzo kikubwa cha mapato yatakayosaidia kuimarisha shughuli mbalimbali za chama.
Kwa mujibu wa Ndg. Abdi, mapato yatokanayo na mali za chama yanaweza kusaidia kulipa stahiki za watumishi, kuendesha shughuli za uongozi pamoja na kurahisisha utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya chama kwa wananchi na wanachama.
Akizungumzia eneo la CCM lililopo katikati ya mji wa Chake Chake, Ndg. Abdi amesema eneo hilo lina thamani kubwa na linaweza kutumika kwa uwekezaji mkubwa utakaoleta manufaa kwa chama.
“Hili eneo la Chake Chake liko mjini kabisa. Kama chama tukilitumia vizuri tunaweza kumpata mwekezaji na kupata fedha nyingi zitakazosaidia kujenga na kuimarisha chama chetu,” amesema.
Aidha, Naibu Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa uongozi wake hautamvumilia kiongozi yeyote wa chama atakayebainika kushiriki au kusaidia watu kujimilikisha maeneo ya CCM kinyume na taratibu.
Amesema ni wajibu wa kila kiongozi na mwanachama kulinda mali za chama na kuhakikisha zinatumika kwa manufaa ya CCM, wanachama na wananchi kwa ujumla.
Ziara hiyo ni ya kwanza kwa Ndg. Abdi Mahamoud Abdi kutembelea na kukagua mali, maeneo na vitegauchumi vinavyomilikiwa na CCM katika Kisiwa cha Pemba tangu alipoteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar.
Amesema chama kinamiliki maeneo ya kimkakati ambayo yakisimamiwa na kutumika ipasavyo yanaweza kuwa chanzo kikubwa cha mapato yatakayosaidia kuimarisha shughuli mbalimbali za chama.
Kwa mujibu wa Ndg. Abdi, mapato yatokanayo na mali za chama yanaweza kusaidia kulipa stahiki za watumishi, kuendesha shughuli za uongozi pamoja na kurahisisha utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya chama kwa wananchi na wanachama.
Akizungumzia eneo la CCM lililopo katikati ya mji wa Chake Chake, Ndg. Abdi amesema eneo hilo lina thamani kubwa na linaweza kutumika kwa uwekezaji mkubwa utakaoleta manufaa kwa chama.
“Hili eneo la Chake Chake liko mjini kabisa. Kama chama tukilitumia vizuri tunaweza kumpata mwekezaji na kupata fedha nyingi zitakazosaidia kujenga na kuimarisha chama chetu,” amesema.
Aidha, Naibu Katibu Mkuu huyo amesisitiza kuwa uongozi wake hautamvumilia kiongozi yeyote wa chama atakayebainika kushiriki au kusaidia watu kujimilikisha maeneo ya CCM kinyume na taratibu.
Amesema ni wajibu wa kila kiongozi na mwanachama kulinda mali za chama na kuhakikisha zinatumika kwa manufaa ya CCM, wanachama na wananchi kwa ujumla.
Ziara hiyo ni ya kwanza kwa Ndg. Abdi Mahamoud Abdi kutembelea na kukagua mali, maeneo na vitegauchumi vinavyomilikiwa na CCM katika Kisiwa cha Pemba tangu alipoteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar.

















0 Comments