6/recent/ticker-posts

Mhe. othman Azungumza na Viongozi wa Chama hicho wa Mkoa wa Kaskazni "B" Unguja Kichama huko Bubwini Mtendeni

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema chama chake kimewaagiza rasmi Wawakilishi wanaotoka chama hicho  kuhakikisha kwamba wanaohoji ipasavyo sambamba na kuwatetea wananchi wote kuhusu haki zao hasa masuala ya ardhi kwa kuwa ni suala lenye malalamiko makubwa Unguja na Pemba.

Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar mstaafu ameyasema hayo huko Bumbwini Mtendeni alipozungunza na viongozi wa chama hicho Mkoa wa Kaskazini ‘B’ Unguja Kichama akiwa kwenye muendelezo wa ziara zake za kuwaeleza viongozi na wananachi masuala mbali mbali yaliyomo kwenye makubaliano yaliyosaini Julai 9 mwaka huu Ikulu Zanzibar

Amesema kwamba wananchi wengi hivi sasa wamekuwa wakilalamikia sana baadhi ya viongozi nchini kuwa na tabia ya kuwanyanganya ardhi zao bila kuwapa fidia kwa kisingizio cha uwekezaji na madai ya kwamba ardhi ni mali ya serikali jambo ambalo sio sahihi.

Amesema kwamba kwa mujibu wa katiba na sheria mbali mbali za Zanzibar Ardhi ni mali ya umma na kwamba serikali inapohitaji kwa matumizi ya maslahi ya umma kunapaswa kufuatwa utaratibu uliopo ikiwa ni pamoja na muhusika kuhusihwa kwenye hatua mbali mbali pamoja na kulipwa fidia anayostakihiki kwa mujibu wa sheria.

mbo kwamba  la mwanzo tunakwenda kupambana nalo kwani kinachofanyika sio haki.

Mhe. Othman amesema kwamba wapo watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakitumia mwanya wa uwekezaji na visingizio vya kwamba aridhi ni mali ya serkali na kuwadhulumu wananchi jambo ambalo linaleta maununguniko makubwa katika kila eneo la Unguja na Pemba.

Amesema chakushangaza wapo maofisa na watendaji wa serikali wamekuwa wakichukua ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji na baadaye kuwauzia wawekezaji jambo ambalo ni dhulma kubwa wanaofanyiwa wananchi hapa Zanzibar.

Aidha amewaeleza viongozi hao kwamba kwamba msimamo wa chama chake hata kama hakijapata madaraka ya kuongoza serikali ni kuahakikisha haki zote za wananchi zinatetea na kulindwa ina inapobidi kutumika mwananchi anayemiliki aridhi analipwa haki yake bila kudhulumiwa kwa mujibu wa sharia.

Amesema kwamba suala hilo  limekuwa likifanywa  kwa njia za ufiusadi na kwamba waliodhulumiwa wote kwa msimamo wa chama chake ni kupatiwa haki yao hata kama ardhi imetumika kwa miaka 20  iliyopita.

Amesema kwamba kwa mujibu wa taratibu zilizopo ardhi inapohitajika kibiashara mwenye kumiliki inabidi akodishe mwenyewe kwa makubaliano na mfanya biashara baada ya wenyewe kuzungunza na kukubaliana na  serikali inapaswa kumsaidia kufanikisha vyema ukodishwaji ho na baadaye  iweze kumtoza kodi kwa mujibu wa sharia.

Amesema kwamba katika taifa lolote ufisadi haujawahi kuwa na mwisho mwema na kuwataka wazanzibari kuukataa ufisadi kwa namna yoyote kwa kuwa ni jambo linaloleta dhulma na kuzuia haki za wengine.

Akizungunzia suala la utumishi wa Umma kujiingiza katika siasa alifahamisha kwamba jambo hilo ni kosa kwa mujibu wa sharia na kwamba zipo nchi nyingi duniani hubadili serikali mara kwa mara lakini utumishi wa umma kwa kuwa ndio roho ya nchi kimaendeleo unabaki kama ulivyo bila kuingizwa kwenye siasa.

Hata hivyo amesema kwamba Zanzibar hali ilivyo sasa ni kinyume kabisa na sharia na tamaduni mbali mbali za siasa kwa kuwa watendaji mbali mbali wamekuwa wakijiingiza kwenye siasa jambo linalokwamisha ufanisi na maendeleo ya nchi.

Amefahamisha kwamba jambo hilo limekuwa likiongeza umasikini kwa wananchi na kwamba huwezi kufanya mwananchi masikini ukitaraji kwamba serikali itakuwa tajiri na kwamba mambo ya namna hiyo ni lazima yarekebishwe kupitia makubaliano hayo.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho upande wa Zanzibar Ismail Jussa Ladhu, amesema kwamba ni vyema wana ACT kuona fahari kubwa na kutembea kifua mbele kwa kuendelea kuilinda Zanzibar na maslahi yake na kuendelea kuwepo na kamwe hawapaswi kuwa wanyonge na kwamba lazima chama chao wakiimarishe na wakijenge e kwa kuwa ndio matumaini ya wananchi wote wazanzibar .

 Watu wanakitegemea chama kwa matarijio ya kuireshea hadfhi Zanzibar lakini pia ni matumaini kwa hali ya maisha yalivyo, na kwamba fakhari ya viongozi kutokana na kuungwa mkono na wananchi wengi wa Zanzibar na wananchi wanaendekea kuwa na ari ya kuipambania Zanzibar.

Amesema kwamba Chama hicho  ni tegemeo pekee la wazanzibar wote hasa kwa hali ya maisha ilivyo sasa kuwa magumu kwa wananchi kwani hali ilivyo sasa watu wote hawanauhakika wa kutimiza mlo wao na iwapo ataumwa hawezi kujitibu, lakini wanaojiita watawala na kujisifu mambo ya namna hiyo hawayajui kwa kuwa hawakuishi maisha ya kinyonge ya watu wa Zanibar.

Amesema kwamba baada ya miaka 60 matabaka yamekuwa makubwa kuliko yalivyokuwa wakati wa ukoloni kila mmoja amejenga makasri na kuwa na magari ya kifahari huku wananchi wakeiendelea kudhoofika nawao wakiwa na maisha ya kifahari.

Amesema kwamba chama hicho kinahoja za kikatiba, kiutawala na kisheria katika kuitetea Zanzibar na kwamba wazee wanapaswa kuwafundisha vijana namna ya kuitea Zanzibar yao kwakuwa wanapambana kupambania Zanzibar na wazanzibari na haki zao.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti mstafu wa chama hicho Taifa Babu Juma Duni Haji, amesema kwamba maisha ya namna ya kufanya uchaguzi kwa vurugu yametosha na kwamba ndio jambo la msingi lilojadiliwa wala sio suala la kugawana vyeo lakini ni kutafuta namna ya kutatua tatizo lililopo Zanzibar  ili masuala ya namna hiyo hatimae yamalizike na yasiwepo Zanzibar.

Mjadala ulilenga Zaidi katika kuweza kuondoa mkasa wa mkanganyiko uliopo na sio wa namna ya kuingia serikali , licha ya kuwepo mjadala mkali na kubishana kwa mas-hara lakini waliweza kufikia hatua na kwamba mungu awezeshe yatekelezwe ili watu waache kuuana

Amefahamisha kwamba haiwezekani kila miaka mitano wazanzibari wanawekwa roho juu na kwamba wazanzibari ni waungwana sio jambo jema watu kuuana kwa kisingizio cha uchaguzi.

Mhe. Othman yupo kwenye ziara yake ya kuzungunza na viongozi mbali mbali wa chama na Jumiya za Kidini kulezea na kuyafafanua masuala mbali mbali yaliyomo kwenye makubaliano hayo iliyoanzia kisiwani Pemba na kesho atazungunza na viongozi wa wilaya za Mjini, Magharib A na B, katika ukumbi wa Majidi Kiembesamaki.

 

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar mstaafu kupitia Kitengo chake cha habari leo Alakhamis Agosti 27, 2026.

Post a Comment

0 Comments