6/recent/ticker-posts

DKT. MWIGULU NCHEMBA AWEZESHA KUTALIWA MGOGORO WA ARDHI ULIODUMU MIAKA 17


Msaidizi wa Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya ardhi, Senso Magesa akishuhudia utiaji saini  maridhiano ya mgogoro wa ardhi kati ya Mfanyabiashara Herse Warsame Mohamed (kushoto) na wananchi watano uliodumu kwa miaka 17 katika eneo la Mtoni Mzinga wilayani Temeke jijini Dar es salaam ambao ulimalizwa kwa njia ya maridhiano na Timu ya Watalaam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Agosti 12, 2026.  Wa tatu kushoto ni kiongozi wa Wananchi hao,  Ivan Kihiyo na kulia ni William Abel Makasi. Wananchi wengine  waliohusika katika maridhiano hayo ni  Hamisi A. Bora, Ramadhani A. Makopa na Sebatian Gervas Rutayuga. 
Mfanyabiashara Hersi Warsame Mohamed  (kushoto) akizungumza kwa furaha na wananchi waliohusika katika mgogoro wa madai ya kudhulumiwa ardhi  na mfanyabiashara  huyo uliodumu kwa miaka 17 katika eneo la Mtoni Kizinga wilayani Temeke  jijini  Dar es salaam  baada ya mgogoro huo kumalizwa kwa njia ya maridhiano na Timu ya Watalaam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Agosti 12, 2026. Wananchi hao ni Bw. Ivan Ruben Kihiyo, Hamisi A. Bora, William Abel Makasi, Ramadhani A. Makopa na Sebatian Gervas Rutayuga
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Post a Comment

0 Comments