Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema ZFF Award ni jukwaa la kutambua juhudi za wanamichezo katika kuleta maendeleo ya michezo, kuenzi vipaji na kuhamasisha ushindani wa michezo.
Ameyasema hayo katika hafla ya ZFF Award msimu wa Nne iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya New Amaani Complex Zanzibar.
Amesema ZFF imepata mafanikio makubwa katika mpira wa Miguu Zanzibar kwa kuboresha utawala wa michezo, kuimarisha mashindano ya ndani pamoja na kuanzisha mifumo ya kisasa ya kidijitali inayoongoza uwazi na ufanisi katika usimamizi wa mpira wa miguu.
Mhe. Hemed amesema kuwa klabu za michezo zinaendelea kuonesha maendeleo makubwa kama vile ushiriki katika mashindano ya Kikanda na Kimataifa jambo linaloitangaza Zanzibar na kuongeza heshima ya nchi katika ramani ya soka.
Makamu wa Pili wa Rais amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya michezo kwa kujenga Uwanja wa Zanzibar Sport City Fumba ikiwa ni sehemu ya matayarisho ya AFCON 2027 ambayo yatatoa fursa nyingi za kiuchumi hapa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Aidha, Mhe. Hemed amesema ujenzi huo wa miundombinu mbali mbali ya michezo ni uthibitisho kuwa Zanzibar imepiga hatua ya maendeleo katika sekta ya michezo na imefanikiwa kupata fursa ya kuandaa mashindano ya viwango vya juu kwa kuwa mwenyeji wa mashindano ya Afcon yanayotarajiwa kufanyika mwakani 2027.
Sambamba na hayo Mhe. Hemed ameipongeza Bodi ya Ligi Kuu ya Zanzibar kwa kushirikiana na ZFF kwa kuchukua hatua stahiki katika kukemea uharibifu wa miundombinu ya michezo sambamba na kuwataka kukaa pamoja na vilabu kuwafahamisha umuhimu wa kuwa na mpira weye viwango na nidhamu ili kuelekea mpira wa ajira tunaoutaka.
Amesema ili kupata wadhami wengi zaidi ni lazima ZFF kukaa na kuangalia mapungu yaliyopo katika soka la Zanzibar kwa vilabu, waamuzi, wakufunzi na wachezaji kisheria na kikanuni na kuyafanyia kazi mapungufu hayo jambo litakakalovutia wadhamini kuja kuekeza katika soka la Zanzibar.
Hata hivyo, metoa wito kwa wananchi wote kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuleta maendeleo sambamba na kuzitumia vyema fursa za kiuchumi zitakazopatikana kupitia mishindano ya Afcon yanayotarajiwa kufanyika mwezi Juni, 2027.
Nae Waziri wa Habari ,Sanaa Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Rizi Pembe Juma amesema kwa kutambua mchango mkubwa wa sekta ya michezo hasa katika kutengeneza ajira kwa vija, Serikali kupitia Wizara ya Habari itaendelea kutoa mashirikia kwa ZFF ili kuhakikisha Mpira wa Zanzibar unaimarika zaidi na kutoa manufaa zaidi.
Dkt. Pembe amewataka wananamichezo na wanananchi wa Zanzibar kuzitumia vyema fursa zitakazopatikana kupitia mashindano ya Afcon yanayotarajiwa kufanyika mwakani 2027.
Kwa upande wake makamu wa rais wa ZFF ndugu Yahya Abdallah shamuni amesema ZFF imeekuwa ikifanya mageuzi makubwa katika usimamizi wa Mpira wa miguu Zanzibar ili kuendana na mabadiliko ya Soka Duniani lakini pia vilabu na wachezaji waweze kupata maendeleo kisoka.
Shamuni ameipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kulingalia soka la Zanzibar kwa upana wake kwa kujenga na kuboresha miundominbu ya michezo ambapo ameiomba Serikali kuandaa utaratibu maalum wa kuvitumia viwanja vya michezo vilivyopo katika kila Wilaya nchini.
Aidha, ameiomba Serikali kuwasaidia katika kupata wadhamini wengi zaidi watakaodhamini ligi mbali mbali nchini jambo litakalosaidia kukuza soka la Zanzibar.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) ndugu Hussein Ahmad Vuai amesema Serikali ya Awamu ya Nane Imeleta mabadiliko makubwa katika Sekta ya Michezo Zanzibar kwa kujengwa viwanja vya michezo kila Wilaya kikiwemo kiwanja cha Afcon ambacho kitaifungua zaidi Zanzibar kimechezo.
Ndugu, amesema katika kutambua michango mbali mbali inayotolewa na wachezaji, wakufunzi na waamuzi wanaotumikia vilabu mbali mbali ZFF imeandaa tuzo hizo za Heshima kama ni chemchem ya kuwaweka pamoja wanamichezo na wadau mbali mbali wa soka kutathmini mustakbali wa soka la Zanzibar.
Akizungumza kwa niaba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya ligi Kuu Tanzania(TPLB) Ndg.Cornel Barnabas amesena TFF imekuwa ikifanya kazi kwa ikishirikiana kwa Karibu na ZFF ili kuhakikisha soka la Tanzani linazidi kuimarika Kitaifa na Kimataifa sambamba na kuangalia maslahi na changamoto zilizopo kwa pande zote mbili na kuzipatia ufumbiuzi.
Cornel amewakumbusha viongozi, wakufunzi, vilabu, wachezaji na wadau wa soka Tanzania kuheshimu na kufuata kanuni na sheria zinazoongoza mpira wa miguu ili soka la Tanzani lizidi kuimarika na kuheshimika duniani kote.
Imetolewa na kitengo cha Habari ( OMPR )
Leo tarehe 09 / 08 / 2026
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
0 Comments