Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kama ishara ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Amali Kizimkazi katika moja ya matukio kuelekea kilele cha Tamasha la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 13 Agosti, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti aina ya Muembe katika Kituo cha Afya Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, tarehe 13 Agosti, 2026. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea mfano wa ufunguo wa gari la wagonjwa kutoka kwa Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani, Kanda ya Afrika, Dkt. Ndoungou Salla Ba, wakati wa ziara fupi ya Rais Dkt. Samia katika Kituo cha Afya Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 13 Agosti, 2026. .jpeg)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Dkt. Saidi Kiangi pamoja na Dkt. Tamim Hamad Said wa Kituo cha Afya Kizimkazi, mfano wa ufunguo wa gari, kama ishara ya makabidhiano ya gari la wagonjwa kwa ajili ya matumizi ya Kituo hicho. Gari hilo lilitolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, katika moja ya matukio kuelekea kilele cha Tamasha la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, tarehe 13 Agosti, 2026. 

.jpeg)


.jpeg)
0 Comments