6/recent/ticker-posts

THUBUB, THRDC yawanoa maofisa SMZ, asasi za kiraia kuhusu haki za binadamu

 

Makamo Mwenyekiti Mstaafu THBUB Mhe. Muhammed Khamis Hamad akizungumza na maofisa wa SMZ na Asasi za kiraia, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo maofisa hao yalifanyika ukumbi wa Ofisi ya Muffti Mkuu wa Zanzibar, iliopo Mazizini Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Mgharibi.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora anayeshughulikia masuala ya Sheria, Bw. Mzee Ali Haji amesema utekelezaji wa haki za binadamu na uimarishaji wa misingi ya utawala bora ni chanzo cha kukuza Amani na Utulivu nchini.

Naibu Mzee ameyasema hayo katika ukumbi wa Ofisi ya Muffti Mkuu wa Zanzibar iliopo Mazizini Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Mgharibi wakati akifungua mafunzo ya siku ya siku mbili ya kuwajengea uwezo watumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Asasi za Kiraia katika kusimamia na kuzilinda haki za binadamu na misingi ya Utawala bora.

Jamii yenye utulivu huvutia uwekezaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa haraka kutokana na usimamizi mzuri wa haki za binadamu na utekelezaji utawala bora kwa kuzingatia sharia. aliifafanua.

Pia alisisitiza suala la ushirikiano wa pamoja baina ya taasisi zinazosimamia sharia akilitaja Jeshi la polisi, vikosi vya Idara Maalum za SMZ hususan JKU Valantia na Magereza kutotumia nguvu kubwa wanapowakama watu.

Aidha, Bw. Ali Haji alizishauri taasisi za haki jinai kuona umuhimu wa kufanya utafiti wa kina kabla ya kufanya maamuzi na kuwachukulia hatua kwa kutumia nguvu kubwa wananchi wananowasimamia ili kuona haki za binadamu zinatekelezwa na utawala bora unasimmamiwa na kuheshimiwa.

“Siku zote ukitaka kuuza uvave viatu vya mnunuzi, kama huwezi kuvivaa basi usiuze” alisisitiza kiongozi huyo.

Mapema akiwasilisha wasilisho la Tume ya haki za binadamu na Utawala Bora kwa watumishi wa SMZ na Asasi za kiraia, Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB) Bw. Msafiri Juma Karibona alisema mbali na majukumu mengi yanayofanywa na Tume hiyo ina jukumu kubwa la kutoa elimu kwa umma ili kuifikia jamii kubwa zaidi kuifunza umuhimu wa kuhifadhi, kuzilinda na kuzisimamia haki za binadamu na misingi ya utawala bora ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupokea malalamiko, kutoa ushauri wa kisheria na kuhimiza uwajibikaji.

Alisema tume pia ina ushirikiano wa karibu na wadau wa mfumo wa haki jinai na asasi za kiraia hasa katika kuhakikisha masuala ya haki za binadamu yanapatiwa majibu kwa wakati na kwa kuzingatia sharia na katiba za nchi.

Akigusia eneo uchunguzi Bw. Karibora alieleza THBUB imepewa mamlaka  kisheia na kikatiba kuchunguza taasisi yoyote inayolalamikiwa na wananchi pia alieleza mipaka ya Tume ya uchunguzi kwa Mhe. Rais wa Zanzinar na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Naye, Makamo Mwenyekiti Mstaafu THBUB Mhe. Muhammed Khamis Hamad akizungumza katika mafunzo hayo alitoa historia ya harakati za kuzipambania haki za binadamu zilivyoanza wakati wa vita vya kwanza na vya pili vya dunia kwa kuzigusia zaidi haki za kiraia na kiuchumi.

Mratibu wa kutoka Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania (THRDC), Bw. Baitani Mujuai, alizisihii sekta zinazosimamia sharia wakiwemo Jeshi la Polisi, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka DPP, ZAECA, Dawa za kulevya, vikosi vya Idara Maalumu za SMZ wakiwemo magereza na mnyororo wote wa haki jinai kukaa pamoja kama familia moja kujadiliana mambo muhimu yanayowahusu watu na haki zao ili kupunguza fujo, mateso kwa watuhumiwa ili kuwa na mahusiano na ushirikiano mzuri baina yao na watu wanaowasimamia kwa kupata jamii yenye kutii sharia.

Akichangia katika mafunzo hayo, Afisa Ulinzi wa Mtoto kutoka Jukwaa la haki za watoto Zanzibar (ZCRF), Ndg. Sharifa Hamad Makame, alieleza kwamba sharia zote za nchi zipo vizuri na zinatekeleza haki za binatamu tatizo liliopo ni katika kuzisimamia na kuzitekeleza kwa baadhi ya wasimamizi wa sharia hizo kwa kuendekeza mbele utashi binafsi.

Mafunzo hayo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo watumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Asasi za Kiraia katika kusimamia na kuzilinda haki za binadamu na misingi ya Utawala bora yaliratibiwa na kufanikishwa na Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania (THRDC) kwa ushirikiano na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, yallifunguliwa na kufungwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora anayeshughulikia masuala ya Sheria, Bw. Mzee Ali Haji Mei 30 – 31, 2026



Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora anayeshughulikia masuala ya Sheria, Bw. Mzee Ali Haji (kushoto) akisalimiana na Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB) Bw. Msafiri Juma Karibona wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo watumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Asasi za Kiraia katika kusimamia na kuzilinda haki za binadamu na misingi ya Utawala bora. Mafunzo hayo yalifanyika ukumbi wa Ofisi ya Muffti Mkuu wa Zanzibar iliopo Mazizini Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Mgharibi.

Naibu Katibu Mtendaji Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB) Bw. Msafiri Juma Karibona, akiwasilisha wasilisho la Tume ya haki za binadamu na Utawala Bora kwa watumishi wa SMZ na Asasi za kiraia, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo maofisa hao yalifanyika ukumbi wa Ofisi ya Muffti Mkuu wa Zanzibar, iliopo Mazizini Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Mgharibi.

Wafanyakazi wa Tume ya haki za binadamu na utawala bora (THBUB)na Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu Tanzania (THRDC) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo maofisa wa SMZ na Asasi za Kiraia yalifanyika ukumbi wa Ofisi ya Muffti Mkuu wa Zanzibar, iliopo Mazizini Wilaya ya Magharibi B Mkoa wa Mjini Mgharibi.

Post a Comment

0 Comments