Na.Mwandishi Wetu Zanzibar.
TIMU ya Madaktari 35 kutoka China imefanya kambi maalum ya matibabu katika Kituo cha SINAI POLY CLINIC Kombeni, ambapo wananchi wamejitokeza kwa wingi kupata huduma mbalimbali za Afya ikiwa ni msaada mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo kutokana na upatikanaji wa huduma za kibingwa na uchunguzi wa haraka wa magonjwa tofauti.
Kambi hiyo imehusisha madaktari bingwa kutoka China kwa kushirikiana na wataalamu wa hapa nchini, ambapo huduma mbalimbali zimetolewa kwa wananchi wakiwemo watoto, wanawake na wazee waliokuwa na uhitaji wa matibabu.
Huduma zilizotolewa ni pamoja na uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya ndani, huduma za macho, afya ya wanawake, meno, upasuaji mdogo pamoja na vipimo vya afya kwa ujumla. Wananchi pia walipata ushauri wa kitaalamu kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza na kuimarisha afya zao za kila siku.
Akizungumzia kambi hiyo, kiongozi wa Timu ya 35 ya madaktari kutoka China BAO ZENGTAO amesema kuwa lengo ni kuimarisha afya za jamii kupitia ushirikiano wa kimataifa kati ya China na Zanzibar, pamoja na kusaidia wananchi kupata huduma bora za afya kwa wakati.
Aidha, alieleza kuwa timu yao imejipanga katika kuwahudumia wananchi katika maeneo mbali mbali kwa lengo la kuimarisha ushirikiano uliopo baina yao huku wakibadilishana ujuzi na wataalamu wa afya wa Zanzibar ili kuongeza ufanisi katika sekta ya afya.
Kiongozi wa Timu ya 35 ya madaktari kutoka China Bao Zengtao
Kwa upande wake, Daktari Dhamana wa Kituo cha SINAI POLY CLINIC KOMBENI Mohamed Ali Mussa katika kambi hiyo ni muhimu sana katika kuinua kiwango cha huduma za afya nchini kwa kuwafikia wananchi moja kwa moja sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani kupitia mafunzo ya vitendo na uzoefu wa moja kwa moja.
Amefahamisha kuwa wataendelea kushirikiana na madaktari hao kwa kuwapatia wananchi huduma ambazo zimeweza kuwafikia kwa karibu huku akiwataka wananchi kufika wanaposikia kunafanyika kambi za matibabu ili kufanya uchunguzi na matibabu ya mapema.
CLIP......Daktari Dhamana wa Kituo cha SINAI POLY CLINIC KOMBENI Mohamed Ali Mussa
Kwa upande wake sheha wa shehia ya kombeni amesema Wananchi wakufurahishwa na huduma hizo, wakisema zimewasaidia kupunguza gharama za matibabu na kuwapa nafasi ya kupata vipimo na dawa bila malipo.
Sheha wa shehia ya kombeni Hamad kombo Wananchi wa Kombeni wameomba kambi kama hizo ziendelee kufanyika mara kwa mara na maeneo mengine ili huduma za afya ziweze kuwafikia kwa urahisi zaidi katika maeneo yao.
.Ameir Ali Amer mwananchi kombeni
Mwisho.
0 Comments