6/recent/ticker-posts

RPC Mkoa wa Kipolisi Temeke Amefanya Matendo ya Huruma kwa Familia Inayozongwa na Maradhi ya Muda Mrefu


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Kungu John Malulu Julai 17,2026 amefanya matendo ya huruma kwa familia ya Matiga iliyopo Kata ya Kijichi jijini Dar es Salaam.

Kamanda Malulu amesema hiyo ni desturi ya Watanzania, kupendana na kujuliana hali, binafsi ameguswa na amewiwa kufanya matendo ya Huruma kwa familia hiyo ambayo imekua ikizongwa na maradhi kwa muda mrefu.

Aidha Kamanda amesema matendo haya ni ya kawaida kwa maafisa wa Jeshi la Polisi kwani hata ukitoa vyeo walivyonavyo ni wa Tanzania wa kawaida hivyo upendo, amani na kujali ndio misingi wanayoishi kila siku.

Naye Diwani wa Kata ya Kijichi Mhe. Tibelyo Exavery Kalinga ameshukuru Utaratibu huo wa Kamanda kwani unafanya Jeshi kua karibu na raia, hivyo huraisisha ile dhana ufichuaji wa wahalifu na uhalifu katika jamii.

Post a Comment

0 Comments