6/recent/ticker-posts

TANZANIA NA BENKI YA ASIA (AIIB) KUSHIRIKIANA KIMKAKATI

Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi (hayupo pichani), kilichofanyika pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo wamejadili kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.


Na Benny Mwaipaja, Washington D.C.

Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na Benki 

ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), hatua 

inayotarajiwa kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya 

kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, 

teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu 

ya kijani.


Hayo yamejiri wakati Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis 

Mussa Omar (Mb), alipo ongoza ujumbe wa Tanzania katika 

kikao na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya 

Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi, pembezoni mwa Mikutano ya 

Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na 

Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, 

nchini Marekani.


Rais wa AIIB, Bi. Zou Jiayi, alisema kuwa Tanzania ni mdau 

muhimu katika Benki hiyo yenye Makao yake Makuu Beijing 

nchini China, na kwamba Benki yake imejipanga kuisaidia 

Serikali kutimiza malengo yaliyopangwa katika utekelezaji wa 

Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.


Aliyataja maeneo yenye kipaumbele kuwa ni pamoja na 

miundombinu ya usafiri wa Reli ya Kisasa, nishati, maji na 

mawasiliano ambapo kupitia uwekezaji huo, benki hiyo 

inalenga kuchochea maendeleo ya miundombinu, kupunguza 

umaskini, kuinua viwango vya maisha ya wananchi na 

kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii.


Kwa upande wake, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis

Mussa Omar (Mb), aliikaribisha Benki hiyo kushirikiana na

Tanzania katika kutekeleza miradi ya upanuzi wa Bandari ya

Dar es Salaam, ujenzi wa Mradi wa Reli iendayo kasi-SGR,

ujenzi wa Bandari ya Mbegani - Bagamoyo na Bandari za

Uvuvi za Zanzibar, Miradi ya kukuza ajira kwa vijana katika

sekta ya teknolojia na miradi mingine ambayo pande hizo

mbili zitakubaliana.




Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi (hayupo pichani), kilichofanyika pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo wamejadili kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.

Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb)(kushoto), na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukutana na kufanya mazungumzo, pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo wamejadili kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Khamis Mussa Omar (Mb) (wa pili kushoto), Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), Bi. Zou Jiayi (Katikati), Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil (Mb) (wa pili kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Aboud Hassan Mwinyi, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe (Spring Meetings) ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo wamejadili kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Washington D.C, Marekani)

Post a Comment

0 Comments