Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi amewasisitiza Mabalozi wanaokwenda Kuiwakilisha Tanzania katika Mataifa mbalimbali kuweka Kipaumbele na kuzingatia Diplomasia ya Kiuchumi kwa kutangaza fursa za Uwekezaji ziliopo Nchini.
Rais DÄ·t, Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 8 Aprili 2026 alipokutana na Mabalozi hao waliofika Ikulu, Zanzibar kumuaga kabla ya kwenda katika Vituo vyao vya Kazi.
Rais DÄ·t, Mwinyi amewahimiza Mabalozi hao kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maslahi ya Pande zote mbili za Muungano na kufahamu kuwa Sera kuu ya Nchi hivi sasa ni Diplomasia ya Kiuchumi.
Amewaeleza Mabalozi hao kwa Zanzibar Sera kuu ni Uchumi wa Buluu unaoambatana na Utalii hivyo ni vema wakaweka Mkazo katika kuwashawishi Wawekezaji kutoka Mataifa hayo kuja kuwekeza Nchini kwani fursa zipo nyingi katika Maeneo mbalimbali ya Uwekezaji.
Rais DÄ·t, Mwinyi amebainisha kuwa Zanzibar iko tayari kupokea Wawekezaji hususani katika Uwekezaji wa Miundombinu ikiwemo Bandari, Viwanja vya Ndege , Barabara, Uvuvi na Utalii.
Eneo jengine ambalo Rais DÄ·t, Mwinyi amesisitiza ni Kupata Wafanyabiashara na Wawekezaji katika Zao la Mwani na Wafanyabiashara watakaowekeza na kununua Karafuu ili kuyaongezea thamani Mazao hayo.
Rais DÄ·t, Mwinyi amewahakikishia Mabalozi hao kuwa Serikali itaweka Mfumo Mzuri zaidi wa Mawasiliano ili kuondosha Urasimu kwa Wawekezaji na kuongeza Ufanisi,
Rais DÄ·t, Mwinyi amewapongeza na kuwatakia Mabalozi hao kila la Heri katika Utekelezaji wa Majukumu yao.
Naye Balozi wa Tanzania Nchini Sweden Balozi Swahiba Mndeme akizungumza kwa Niaba ya Mabalozi hao amemuhakikishia Rais Dkt Mwinyi kuyapokea na kuyatekeleza Maelekezo yake kwa Vitendo na kuitangaza Diplomasia ya Uchumi Kikamilifu.
Mabalozi.walioaga ni Balozi,Mhandisi Zena Ahmed Said -Saudi Arabia, Balozi Cyprian John Luhemeja -Zambia ,Balozi Maulida Bwanaheri Hassan-Oman,Balozi Salim Othman Hamad-Comoros,Balozi Swahiba Mndeme-Sweden, Balozi Noel Emmanuel Kaganda-Korea na Balozi Mussa Haji Ali ,Naibu Mwakilishi wa Kudumu Umoja wa Mataifa-New York.


0 Comments