6/recent/ticker-posts

MHE BALOZI OMAR AKUTANA NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA IMF KUJADILIATHARI ZA VITA YA MAREKANI-ISRAEL NA IRAN

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, Bw. Adran Ubisse, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika ofisi za Shirika hilo, pembezoni mwa Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo walijadiliana namna ya kukabiliana na athari za mizozo ya kivita inayoendelea duniani ikiwemo Mashariki ya Kati, inayotishia ustawi wa uchumi wa dunia.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil (wa tatu kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, Bw. Adran Ubisse (wa tatu kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa pili kulia), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi (kulia), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Balozi Elsie Sia Kanza (wa pili kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika ofisi za IMF, pembezoni mwa Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo walijadiliana namna ya kukabiliana na athari za mizozo ya kivita inayoendelea duniani ikiwemo Mashariki ya Kati, inayotishia ustawi wa uchumi wa dunia.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Wa tatu kulia), Waziri wa Fedha na Mipango kutoka Ofisi ya Rais-Zanzibar, Mhe. Dkt. Juma Malik Akil (wa tatu kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF anayesimamia Idara ya Afrika, Bw. Abebe Selassie (Katikati), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF anayesimamia Idara ya Afrika, Bw. Abebe Selassie, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (wa pili kushoto), Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, Bw. Aboud Hassan Mwinyi (kushoto), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba (wa pili kulia) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Balozi Elsie Sia Kanza (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika ofisi za IMF, pembezoni mwa Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na IMF (2026 IMF/WBG Spring Meetings) inayofanyika, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambapo walijadiliana namna ya kukabiliana na athari za mizozo ya kivita inayoendelea duniani ikiwemo Mashariki ya Kati, inayotishia ustawi wa uchumi wa dunia.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, jijini Washington D.C, Marekani)
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, jijini Washington D.C, Marekani)

 

Post a Comment

0 Comments