Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akimkabidhi Tunzo Mama Fatma Karume, ya kutambua mchango wake katika uwezeshaji wa wanawake iliyotolewa na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL ) katika hafla ya Jukwaa la The Citezen Woman Rising 2026 lilofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar..jpeg)
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuweka mazingira bora kwa wanawake ili kuwainua kiuchumi na kuwashirikisha katika nafasi za maamuzi kama Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025.2030 na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050 zinavyoelekeza.
Ameyasema hayo kwa Niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi katika hafla ya ugawaji wa zawadi katika Jukwaa la The Citezen Rising Women Zanzibar Edition 2026, hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Zanzibar.
Amesema jukwaa la the Citizen Rising Women limelenga kutambua nafasi ya Mwanamke katika kuleta maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii na kuwa mstari wa mbele katika kuchangia ukiwaji wa uchumi wa Taifa.
Amefahamisha kuwa Serikali kupitia wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar (ZEEA) kwa kipindi chwa mwaka 2022 hadi kufikia mwezi Machi 2026, imefanikiwa kutoa mikopo isiyo na riba na yenye masharti nafuu yenye thamani zaidi ya shilingi za Kitanzania Bilioni 53 kwa Unguja na Pemba ambapo wanawake pekee walionufaika na mikopp hiyo ni asilimia 83.6
Aidha, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kati ya wananchi 15,609 waliopatiwa mafunzo ya ujasiriamali asilimia 75 ni wanawake ambao wamenufaika kwa kujifunza kusarifu na kutengeneza bidhaa mbalimbali ikiwemo mboga mboga na matunda, sabuni, ufugaji wa nyuki, masoko ya kidijitali, elimu ya fedha na mengineyo.
Sambamba na hayoa Mhe. Hemed amesema katika kutambua na kuthamini mchango wa mwanamke, Serikali imeweka maeneo ya kimkakati kwa lengo la kumyanyua mwanamke ikiwemo kuimarisha mifumo ya uwezeshaji wanawake kiuchumi pamoja na kuimarisha mifumo ya kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia kwa kuboresha zaidi madawati ya kijinsia.
Hata hivyo, Serikali imeanzisha na kuimarisha mitandao ya wanawake ili kusaidia kubadilishana maarifa, fursa za maendeleo na kuimarisha zaidi ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi kwenye sekta za Umma na sekta binafsi.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Mhe. Zawadi Amour Nassor amesema wanawake wamekuwa na mchango mkubwa katika kulijenga Taifa hivyo kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kuekeza nguvu zake katika kumnyanyua na kumuwezesha mwanamke hasa mtoto wa kike ili aweze kusimamia na kutimiza ndoto zake alizojiwekea.
Mhe. Zawadi amefahamisha kuwa wakati umefika kwa jamii kuachana na mitazamo hasi ambayo inamkandamiza mwanamke na kuwataka kuungana pamoja katika kuwawezesha wanawake hasa wale ambao tayari wamejiwekeza katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Hivyo ameyaomba Mashirika na Taasisi mbali mbali kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwanyanyua na kuwawezesha wanawake kiuchumi jambo ambalo litaliwezesha Taifa kuzidi kupiga hatua kimaendeleo.
Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communicans Limited (MCL) ambao ndio waandaaji wa Jukwaa la The Citezen Rising Woman 2026, Bi.Rosalyn Mndolwa Mworia amesema wameamua kulileta Jukwaa hilo Zanzibar wakiwa na lengo la kushirikiana na Serikali katika kupaza sauti na kutanua wigo wa kumuwezesha mwanamke kutimiza ndoto zake.
Rosalyn amesema Jukwaa hilo limekuwa ni kichocheo kikubwa cha kuwanyanyua wanawake katika uchumi, Siasa na Uwekezaji jambo ambalo limepunguza changamoto ya kuwepo kwa wimbi kubwa la wanawake tegemezi.
Amefahamisha kuwa MCL itaendelea kupaza sauti na kuwaunganisha wananchi katika kuchochea mabadiliko chanya ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hasa kwa upande wa wanawake ambao wengi wao sauti zao zimekosa kusikika kwa waliowategemea kuwanyanyua na kuwaonesha njia ya mafanikio.
Mapema Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa uwezeshaji wananchi kiuchumi Zanzibar (ZEEA) ndugu Juma Burhan amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanikiwa kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapatia mikopo nafuu ambayo imewawezesha kujishughulisha na miradi mbali mbali inayowakwamua na umasikini.
Burhan amesema mbali na mikopo isiyo nariba, ZEEA imekuwa ikiwapatia elimu ya fedha na mafunzo mbali mbali wajasiriamali wadodo wadogo na wakati ambapo zaidi ya asilimia 60 ni wanawake.
%20(1).jpeg)
Imetolewa na Kitengo cha Habari ( OMPR )
Leo tarehe 16 / 04 / 2026
.jpeg)
.jpeg)
%20(1).jpeg)
.jpeg)
0 Comments