Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema ataendelea na utaratibu wake wa kuwapatia Iftari watumishi wa Chama cha Mapinduzi kila ifikapo mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Hayo yameelezwa kwa niaba yake na Ndugu ALI YUSSUF SALUM msaidizi wa Makamu wa Pili wa Rais katika masuala ya siasa wakati akikabidhi ftari kwa watumishi wa CCM ngazi ya Wilaya na Mikoa hafla iliyofanyika Ofisi kuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui.
Amesema imekuwa ni utamaduni wa Makamu wa Pili wa Rais kila ifikapo mwezi wa Ramadhani kugawa Iftari kwa makundi mbali mbali wakiwemo watumishi wa Chama Cha Mapinduzi Unguja na Pemba jambo ambalo linazidi kuwaweka karibu watumishi na viongozi wao.
Aidha Bwana Ali Yussuf amesema kupatiwa iftari hizo kwa watumishi wa chama kunalenga kuzidisha umoja na ushirikiano kati ya watumishi na viongozi wao ambapo jumla ya watumishi 450 wa Chama na Jumuiya zake wamekabidhiwa Iftari hizo ambazo zinajumuisha mchele, Unga wa ngano na mafuta yakupikia.
Akizungumza kwa Niaba ya Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Katibu wa Uchumi na Fedha Ndugu Afadhali Taib Afadhali amewataka Makatibu wa CCM wa Wilaya na Mikoa kuhakikisha wanazigawa iftari hizo kwa walengwa na kuhakikisha zoezi hilo linakamilika pasipo na usumbufu wa aina yoyote ile.
Ndugu Afadhali amefahamisha kuwa azma ya viongozi wa CCM ni kuhakikisha wanawawekea mazingira mazuri watumishi wa chama pamoja na kuwajenga kuwa na umoja, upendo na mshikamano wakati wote ndani na nje ya chama ili kulinda hadhi na heshima ya chama cha mapinduzi.
Kwa upande wake Katibu Idara ya Siasa, Itikadi, Uwenezi na Mafunzo ya chama komred Khamis Mbeto Khamis amemshukuru Makamu wa Pili wa Rais kwa kuendeleza utamaduni wake wa kuftari pamoja na watumishi wa Chama cha Mapinduzi kila ifikapo mwezi wa Ramadhani jambo linalodhihirisha upendo alionao kwa watendaji wa CCM na Jumuiya zake.
Komred Mbeto amesema wamepokea iftari hizo na kuahidi kuwa zitawafikia walengwa kama ilivyokusudiwa ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa ya kutolewa kwa iftari hizo.
Akizungumza kwa naiba ya makatibu wenzake Katibu wa CCM wilaya ya Mjini ndugu Bilal Hassan Maulid amemshukuru na kumpongeza Makamu wa Pili wa Rais kwa upendo na msikamamo alionao kwa watumishi wa chama hicho kwa kuendelea kuftari pamoja na watumishi hao na kuahidi kuwa ftari hizo watazifikisha kwa walengwa kama ilivyokusudiwa na kiongozi huyo.
Imetolewa na kitengo cha Habari ( OMPR )
Leo tarehe …11 / 03 / 2026
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
0 Comments