Na Idara ya Habari Maelezo Zanzibar. 23.07.2026
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga kujenga uwelewa kwa wananchi juu matumizi ya teknolojia na akili unde (AI) ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya mtandao wa teknolojia ya habari na mawasiliano.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga kuhusu Jukwaa la Kimataifa la teknolojia na akili unde (AI) katika ukumbi wa Tume ya Uchaguzi Maisara Mkoa wa Mjini magharib.
Amesema katika kuhakikisha Serikali inaenda sambamba na mabadiliko ya kijijitali ni vyema kuandaa jukwaa hilo ambalo litawasilisha ajenda zitakazoleta uwelewa kwa jamii na kua sauti ya kuwasilisha maudhui ya mpango wa mageuzi ya kijijitali katika visiwa vya Zanzibar.
“Hatuwezi tukabaki nyuma katika suala zima la tehama na matumizi ya mfumo na masuala ya kijitalaization, hii ni foram ambayo italeta taswira ya kikanda na kimataifa”.amefafanua Waziri Soraga
Hata hivyo amefafanua kuwa jukwaa hilo litasaidia kuleta fursa ya kukutanisha wadau wa nje na wa ndani katika sekta mbalimbali pamoja na kuwekeza katika masuala ya tehama na mifumo ambayo inatatua changamoto katika jamii.
Vilevile Waziri Soraga amewataka wadau wa tehama na kampuni ambazo zinajishughulisha na mifumo ya kijijitali pamoja na Wanafunzi ambao wanajikita katika masomo ya tehama na mifumo kushiriki katika jukwaa hilo kwa ajili kupata uwelewa na leta maendeleo katika Nchi.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa UniqTouch Ndg Edwin Robert George amesema jukwaa hilo linakwenda kuwa historia ambayo itakuza na kuendeleza nafasi ya Zanzibar katika teknolojia na ubunifu barani Afrika.
Hata hivyo ameongezea kuwa jukwaa hilo litasaidia Wafanyabiashara na kampuni zinazoendesha mifumo ya tehama kuweza kujua jinsi ya kuendesha biashara zao kupitiaa mfumo hiyo na kuendeleza jamii pamoja na kuwa na uchumi imara wa kijijitali.
Nae Mkurugenzi Idara ya Ubunifu kutoka Wizara ya Mawasiliano,Teknolojia ya Habari na Ubunifu Zanzibar Ndg Samora John Chacha amesema jukwaa hilo ni chachu katika nchi kwani litaleta maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Utalii na Mawasiliano.
Jukwaa hilo la kimataifa linatarajiwa kufanyika kuanzia Septemba 24-26 mwaka 2026 lenye kauli mbiu ya Afrika innovates na kushirikisha wadau kutoka mataifa mbalimbali duniani.
0 Comments