Msimamizi wa Uchaguzi wa Viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa ambaye pia ni Msajili Msaidizi, Bw. Sisty Nyahoza akisoma kanuni zinazoongoza Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa viongozi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Waliokaa kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. Muhiddin Mapeyo, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mh. Mohammed Ali Ahmed na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mstaafu, Mhe. Francis Mutungi.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mstaafu, Mhe. Francis Mutungi akifafanua jambo wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Waliokaa kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw. Muhiddin Mapeyo, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Mh. Mohammed Ali Ahmed na kulia ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa ambaye pia ni Msajili Msaidizi, Bw. Sisty Nyahoza.
Wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa wakipiga kura wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vya uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Uchaguzi umekamilika kwa Mhe. Juma Ali Khatibu kutetea kiti cha Uenyekiti kwa kupata kura 30 za ndiyo dhidi ya kura moja iliyoharibika huku Makamu wake akiwa ni Mhe. John Mongella ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzzi (CCM) Bara baada ya kupata ushindi wa kura 30 za ndiyo dhidi ya kura moja ya Hapana.
Kamati ya kusimamia Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa ikiongozwa na Msimamizi wa Uchaguzi huo, Bw. Sisty Nyahoza wakiwa katuika zoezi la kuhesabu kura wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa baraza hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Uchaguzi umekamilika kwa Mhe. Juma Ali Khatibu kutetea kiti cha cha Uenyekiti kwa kupata kura 30 za ndiyo dhidi ya kura moja iliyoharibika huku Makamu wake akiwa ni Mhe. John Mongella ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzzi (CCM) Bara baada ya kupata ushindi wa kura 30 za ndiyo dhidi ya kura moja ya Hapana.
Msimamizi wa Uchaguzi wa Viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa ambaye pia ni Msajili Msaidizi, Bw. Sisty Nyahoza akionyesha kura iliyoharibika mara baada ya zoezi la kuhesabu kura za Mgombea wa Uwenyekiti wa Baraza hilo wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa viongozi hao uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Kutoka kushoto ni Wajumbe wa Sekretarieti OMVVS, Bw. Laurent Mnaku, Muhiddin Mapeyo na Wakala wa Mgombea Bw. Abdul Mluya.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Dimwa akimwakilisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara , Komredi John Mongella wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026. Katika uchaguzi huo Mongella ameshinda kiti cha Makamu Mwenyekiti kwa kupata ushindi wa kura 30 za ndiyo dhidi ya kura moja ya Hapana.
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Mhe. Juma Ali Khatib akitoa neno la shukrani mara baada ya kuchaguliwa tena kuongoza Baraza hilo kufuatia ushindi wa kura 30 kati ya 31 sawa na 96.8% za kura zote zilizopigwa. Uchaguzi huo ulihusisha uchaguzi wa Mwenyekiti pamoja na Makamu wake ambapo Mhe. John Mongela ametetea kiti chake pia hivyo wataendelea kuongoza baraza hilo kwa kipindi cha miaka miwili tena.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa wakifuatilia mchakato wa Uchaguzi wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Vyama vya Siasa wakifuatilia mchakato wa Uchaguzi wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa ajili ya Uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Ukumbi wa Nashera Hotel Mjini Morogoro tarehe 23 Julai, 2026 (Picha na ORPP).








0 Comments