6/recent/ticker-posts

Rais Mhe. Dkt. Samia ahutubia Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Urusi, lililofanyika St. Petersburg nchini humo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Urusi lililofanyika Jijini St. Petersburg nchini Urusi tarehe 05 Juni, 2026. Kongamano hilo limewakutanisha Wafanyabiashara, Wawekezaji pamoja na Taasisi za kukuza Uwekezaji kutoka Tanzania na Urusi. 


Na Beda Msimbe,TBN, Petersburg, Urusi
Ushirikiano wa miaka 65 ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi sasa unatafsiriwa kuwa daraja imara la maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku sekta ya utalii ikichukua mwelekeo mpya wa kimkakati kuvutia masoko ya kimataifa likiwemo la Urusi. 
Alisema anatambua soko la Urusi ni kubwa naTanzania ipo tayari kulihudumia kwa kuondoa vikwazo kadhaa ikiwamo kuwezesha kupatikana kwa safari za moja kwa moja kutoka Moscow hadi Dar es Salaam na Zanzibar.
Rais alisema hayo wakati akihutubia wawakilishi kutoka nchi 130 duniani zilizoshiriki mkutano wa kiuchumi wa kimkataifa wa Petersburg Juni 5, 2026.
Katika jukwaa hilo la kiuchumi, Rais  Samia  alitangaza kuwa kuanzia Julai 2 mwaka huu, Shirika la Ndege la Tanzania, Air Tanzania, litaanza safari za moja kwa moja kati ya Dar es Salaam, Moscow, na Zanzibar kwa lengo la kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia laki tano ifikapo mwaka 2030 na hatimaye milioni moja. 
Hatua hii inaenda sambamba na ushindi wa tuzo za kimataifa ambapo hifadhi ya Serengeti imetajwa kuwa bora zaidi Afrika na Zanzibar kupewa tuzo kama eneo bora la mikutano na mapumziko. 
Rais Samia alihitimisha kwa kutoa rai kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa na nchi za Afrika ziko tayari kukua kupitia mifumo yao kama soko huru la Afrika, akisisitiza kuwa Tanzania imefungua milango yote kwa wabunifu na wafanyabiashara wanaotaka kushiriki katika safari hii mpya ya mabadiliko.







Post a Comment

0 Comments