|
Hospitali za Serikalii na binafai zimetakiwa kuitumia Wakala wa Vipimo Zanzibar ili kudhibitisha mizani zao na kutoa huduma za matibabu ya vipomo kwa usahihi
Mwamasheria kutoka Wakala wa Vipimo Zanzibar ambae pia ni Kaimu Mkurugenzi Rukia Mkali Fadhil ametoa wito huo katika Hospitali ya Wilaya Ijitimai Wilaya ya Magharibi B* mara bada ya ghafla ya upimaji wa mizani mbalimbali za matibabu kwa ajili ya udhibitisho iikiwa ni shamrashamea za kuelekea kilele Cha maadhimisho ya siku ya Vipimo duniani
Amesema kuwa kufanya hivyo kutaisaidia kudhibitisha mizani na kutoa huduma kwa usahihi sambamba na jamii kupata uwelewa wa kufahamu kazi zinazofanywa na Wakala wa Vipomo
Aidha amefahamisha kuwa Zanzibar ni sehemu ya dunia hivyo kuadhimisha siku hiyo ni muhimu kwani ipo haja kwa jamii kuionesha kwamba mizani zinazotumika zinakua sahihi na za vymba hakika
Ameongeza kuwa suala la vipomo ni suala mtambuka kwani vipomo vinatumika katika maisha ya kila siku
Nae Daktari Dhamana Msaidizi wa Haspitali ya Wilaya Ijitimai Abdallah Khamis Machano amesema ujio wakala wa vipomo hospitalini hapo ni udhibitisho tosha wa upimaji wa mizani mbalimbali kwa usahihi
Aidha amewataka wakala hao kuendelea kutembelea maeneo mbali kwa ajili ya upimaji ili kutambua na kupata ubora wa vipimo hivyo
Katika upimaji huo mizani sita zimedhibitiahwa na kuonekana ziko sahihi
0 Comments