6/recent/ticker-posts

Wakala wa Vipimo Wafika Ijitimai Kupima Mizani


Idara ya Habari (MAELEZO) Maelezo Zanzibar

Hospitali za Serikalii  na binafai zimetakiwa kuitumia Wakala wa Vipimo Zanzibar ili kudhibitisha mizani zao na kutoa huduma za matibabu ya vipomo  kwa usahihi

Mwamasheria kutoka Wakala wa Vipimo Zanzibar ambae pia  ni Kaimu Mkurugenzi Rukia  Mkali Fadhil ametoa wito huo katika  Hospitali ya Wilaya Ijitimai Wilaya ya Magharibi B* mara bada ya ghafla ya upimaji wa mizani mbalimbali za matibabu kwa ajili ya udhibitisho iikiwa ni shamrashamea za kuelekea kilele Cha maadhimisho ya siku ya Vipimo duniani

Amesema kuwa kufanya hivyo kutaisaidia kudhibitisha mizani na kutoa huduma kwa usahihi sambamba na  jamii kupata uwelewa wa kufahamu kazi zinazofanywa na   Wakala wa Vipomo 

Aidha amefahamisha kuwa Zanzibar ni sehemu ya dunia hivyo kuadhimisha siku hiyo ni muhimu kwani  ipo haja kwa jamii kuionesha  kwamba mizani zinazotumika zinakua sahihi na za vymba hakika

Ameongeza kuwa suala la vipomo ni suala mtambuka kwani vipomo vinatumika katika maisha ya kila siku

Nae Daktari Dhamana Msaidizi wa Haspitali ya Wilaya Ijitimai Abdallah Khamis Machano  amesema ujio  wakala wa vipomo hospitalini hapo ni udhibitisho tosha wa upimaji wa mizani mbalimbali kwa usahihi

 Aidha amewataka wakala hao kuendelea kutembelea maeneo mbali kwa ajili ya upimaji ili kutambua na  kupata ubora wa vipimo hivyo

Katika upimaji huo mizani sita zimedhibitiahwa na kuonekana ziko sahihi  

Post a Comment

0 Comments