6/recent/ticker-posts

RAIS DKT. MWINYI: SMZ KUENDELEA KUIMARISHA HUDUMA ZA HIJJA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akizungumza leo, tarehe 03 Mei 2026, wakati wa hafla ya kuwaaga mahujaji wanaokwenda kutekeleza ibada ya Hijja Makkah, Saudi Arabia, iliyofanyika katika Msikiti wa Jamiu Zinjibar, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali kupitia Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana itaendelea kuimarisha huduma za Hijja na kushughulikia changamoto zinazowakabili mahujaji.

Akizungumza leo, tarehe 03 Mei 2026, katika hafla ya kuwaaga mahujaji wanaokwenda Makkah, Saudi Arabia, iliyofanyika Msikiti wa Jamiu Zinjibar, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi. 

Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa ibada ya Hijja kama Nguzo ya Tano ya Uislamu na kuwataka mahujaji kudumisha nidhamu na mwenendo mwema.

Amesema Zanzibar imeendelea kupata mafanikio katika usimamizi wa Hijja kila mwaka, hali inayochangia kuongezeka kwa idadi ya mahujaji.

Halikadhalika, ameishukuru Serikali ya Saudi Arabia, taasisi zinazohudumia Hijja, Shirika la Ndege la Saudi Arabia pamoja na Ubalozi wa Tanzania kwa mchango wao katika kuhakikisha huduma bora kwa mahujaji wa Zanzibar.

Rais Dkt. Mwinyi ameongeza kuwa Serikali inaendelea kukamilisha hatua za kisheria kuimarisha Mfuko wa Hijja wa Zanzibar ili kuongeza fursa kwa wananchi wengi zaidi kushiriki ibada hiyo.

Vilevile, amesifu ushirikiano wa Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana, Umoja wa Taasisi za Hijja Zanzibar pamoja na wadau mbalimbali kwa mchango wao katika kufanikisha safari za Hijja.









Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akizungumza leo, tarehe 03 Mei 2026, wakati wa hafla ya kuwaaga mahujaji wanaokwenda kutekeleza ibada ya Hijja Makkah, Saudi Arabia, iliyofanyika katika Msikiti wa Jamiu Zinjibar, Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi

Post a Comment

0 Comments