6/recent/ticker-posts

Watuhumiwa 40 washikiliwa na Jeshi la Polisi Zanzibar.


Hivi karibuni kumejitokeza tabia ya baadhi ya watu kuwatuhumu watu wengine kuwa, wamewashika mabega na sehemu zao za siri kutoweka.

Taarifa hizi zisizo na ukweli zinazohusishwa na imani za kishirikina zimezua taharuki kubwa katika jamii na kusababisha madhara ikiwa majeruhi na kifo.

Jumla ya matukio 29 yameripotiwa kutokea katika Mikoa minne ya Zanzibar, Mkoa wa Mjini Magharib matukio 22, Mkoa wa Kusini Unguja tukio 1, Mkoa wa Kusini Pemba matukio matatau(3) na Mkoa wa Kaskazini Pemba matukio matatu(3).

Ambapo katika matukio matatu ya Mkoa wa Kaskazini Pemba  tukio 1 limesababisha kifo cha mtu mmoja alifahamika kwa jina la Hamad Othman Mwalim (35) Mkazi wa kijiji cha Jojo watuhumiwa watukio hilo tayari wanashikiliwa na Jeshi la Polisi.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi linawashikilia Jumla ya watuhimiwa arubaini(40) na baadhi yao wamefikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazo wakabili.

Vilele, kwenye matukio yote hayo yaliripotiwa wahusika waliodai sehemu zao za siri zimepotea, Jeshi la Polisi limewafikishwa hospitali na kufanyiwa uchunguzi na Madaktari na kubainika kua sehemu zao za siri zipo na hakuna athari yoyote waliyokua nayo.

Jeshi la Polisi linawasihi wananchi kupuuza uvumi huo na kuacha kusambaza taarifa zisizothibitishwa, kwani kufanya hivyo kunaweza kuvuruga amani na utulivu uliopo katika  jamii.

Aidha, mtu yeyote atakayebainika kuhusika katika kusambaza taarifa za uongo kwa makusudi na kutia taharuki katika jamii atachukuliwa hatua za kisheria.

Jeshi la Polisi linaendele kuwasihi wananchi kutoa taarifa sahihi pale wanapobaini viashiria vyovyote vya uhalifu,kuacha kuchukua sheria mikononi na kutumia vyanzo rasmi kupata habari zilizo sahihi.

Imetolewa na Kamishna wa Polisi Zanzibar,

Makao makuu ya  Polisi Zanzibar.

Post a Comment

0 Comments