Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji, Mhe Shaaban Ali Othman ameahidi kutoa Shilingi Milioni 30 ikiwa ni zawadi za mshindi wa kwanza na wapili wa Ligi Kuu ya Vijana U-21 Zanzibar.
Waziri Shaaban ametoa ahadi hiyo katika mchezo wa ufunguzi wa ligi hiyo kati ya Timu ya Mafunzo U-21 dhidi ya KVZ U-21 katika viwanja vya Mau.
Amesema Bingwa wa Ligi hiyo atakabidhiwa milioni 20 na mshindi wa pili milioni 10 ikiwa ni moja ya hamasa ya kukuza vipaji pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa vijana.
Amesema Vijana wana nafasi kubwa ya kutumia sekta ya michezo ili kujiajiri kwani Serikali imekuwa mstari wa mbele kuwaunga mkono pamoja na kuwawekea mazingira mazuri ili kufikia malengo yao.
Ligi hiyo msimu huu itashirikisha timu 7 ambazo ni Mafunzo, KVZ, Zimamoto, KMKM, JKU, Kipanga na Uhamiaji.
















0 Comments