6/recent/ticker-posts

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR --ZIARA YA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO --MKOA WA KUSINI UNGUJA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza kwa njia ya simu na Meneja Mkuu wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) Mhandisi Haji Haji kutaka kufahamu shirika limejipangaje katika kutatua changamoto ya umeme mdogo inayowakabili wananchi wa Kijiji cha Muyuni na vitongoji vyake, mazungumzo hayo yamefanyika mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Muyuni A Branch  hadi Muyuni C branch .

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Serikali imejipanga kuwalipa fidia wananchi wote ambao makaazi yao yamepitiwa na ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miramdi ya Maendelea inayojengwa katika Mkoa wa Kusini Unguja.

Akikagua ujenzi wa Barabara ya  Muyumi A branch hadi Muyuni C branch Mhe. Hemed amesema suala la fidia linaendelea kufanyiwa kazi na muda mfufi ujao kutoka sasa wananchi watalipwa fidia zao ili kupisha ujenzi wa barabara hizo na miradi mengi inayoendelea kujengwa.

Aidha amewataka wananchi wa muyuni kuitunza misingi ya kupitishia maji inayonjengwa pembezoni mwa barabara hizo ili kujiepusha na athari za Kiafya na kimazingira pindi mitaro hio itakapoziba.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe.Dkt Khalid Salum Muhammed amewataka wananchi wa muyuni na vitongoji vyake  kuwasilisha changamoto zao katika wizara husika ili yaweze kupatiwa utatuzi wa haraka.

Dkt. Khalid amesema dhamira ya Wizara ya Ujenzi na uchukuzi ni kuwalipa wananchi fidia zao kabla ya kuanza kwa ujenzi wa miradi inayoendelea kujengwa nchini ambapo amewaahidi wananchi kuwa taratibu za ulipwaji wa fidia zimefikia hatua nzuri na muda mfupi ujao watalipwa na kupisha wakandarasi kuendelea na ujenzi.

Mkandarasi kutoka Wizara ya Ujenzi na uchukuzi Mhandisi Hamad Juma Omar amesema ujenzi wa Barabara ya Muyuni A branji hadi Muyuni C branji yenye urefu wa Kilomita 3.37 hadi kukamilika kwake utagharimu Dola Za Kimarekani Milioni 2.89 ambao unatarajiwa kumalizika mwezi Mei ( 5 ) mwaka huu.

Kwa upande wao wananchi wa kijiji cha Muyuni wameiomba Serikali kuwajengea barabara zao za asili ambazo bado zinaendelea kutumika pamoja na kulipwa fidia zao ili waweze kupisha ujenzi wa barabara hizo ambazo zitafungua fursa mbali mbali za kiuchumi na za kijamii.

Katika hatua nyengine Makamu wa Pili wa rais wa Zanzibar ametembelea ujenzi wa barabara na daraja la UZI NG'AMBWA ambapo aliwataka wakandarasi kuhakikisha kuwa miradi hio inajengwa kwa viwango na ubora uliokusudiwa pamoja na kukamilila kwa wakati uliopangwa na Serikali ili wananchi wanufaike na miradi hio.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa barabara na daraja la uzi Ng'ambwa utatatua changamoto ya usafiri na uafirishaji , kuongezeka kwa thamani ya ardhi katika kijiji hicho pamoja na kifungua milango ya uwekezaji.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitembelea ujenzi wa mradi wa tangi la kuhifadhia maji kizimkazi Mkunguni kituo cha kupokelea na kupozea Umeme kilichopo Kijini Makunduchi ambacho kitataua kwa kiasi kikubwa changamoto za upatikanaji wa umeme hasa kwa mkoa wa kusini.

Amesema kukamilika kwa ujenzi wa Miradi hio wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja wataondokana na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama na kuondokana na changamoto ya  kukatika umeme mara kwa mara pamoja na kuwepo kwa umeme mdogo kwa baadhi ya maeneo sambamba na kukua na kuimarika kwa shughuli za biashara katika maeneo hayo.

Miradi mengine iliyokaguliwa na   Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ni ujenzi wa Dakhalia ya Skuli ya Sekondari ya Hasnu Makame,Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mama na Mtoto MakunduchiUjenzi wa Madarasa 30 katika Skuli ya Jumbi na Ujenzi wa Barabara za Ndani Kikungwi na Mradi wa Maji Kidimni.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisikiliza kero za wananchi  wa Kizimkazi mara baada ya kukagua ujenzi wa Tangi la Kuhifadhia maji linalojengwa katika kijiji cha Kizimkazi Mkunguni.



Imetolewa na Kiengo cha Habari ( OMPR )

 Leo tarehe   19  /  04  / 2026

Post a Comment

0 Comments