Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa katika ufungaji wa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wajumbe hao yaliyofanyika katika Ukumbi wa Makao Makuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui..jpeg)
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Hemed Suleiman Abdulla amesema umoja, mshikamano na nidhamu uliomo ndani chama cha Mapinduzi ndio silaha pekee ya kuzidi kikiimarisha chama hicho.
Ameyasema hayo wakati wa ufungaji wa mafunzo maalum kwa wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa katika Ukumbi wa Mkao Makuu ya CCM Zanzibar Kisiwandui.
Amesma kupitia mafunzo hayo kutazidisha kuimarika kwa umoja, mshikamano na nidhamu ndani ya chama ambako ndiko kunakopelekea chama kupata ushindi siku hadi siku.
Aidha amefahamisha kuwa uadilifu na uwajibikaji ni jambo la msingi ndani ya chama ambalo huwajengea Imani wanachama kwa viongozi wao hasa katika kutekeleza shughuli mbali mbali za chama.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewakumbusha washiriki hao kutambua kuwa viongozi ndio walinzi wa taarifa nyeti za chama ambapo kuvuja kwa taarifa hudhoofisha mshikamano na ustawi wa chama.
Hata hivyo, Mhe. Hemed amewaasa wajumbe wa mafunzo hayo kuwa makini na kwenda kuyatekeleza kwa vitendo yale yote ambayo wamejifunza kwani kufanya hivyo kutapelekea kufanya vizuri katika kazi zao ikiwemo kukitetea chama cha mapinduzi.
Nao washiriki wa mafunzo hayo wameushukuru uongozi wa chama cha mapinduzi kupitia Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar kwa kuwaandalia mafunzo hayo ambayo yanawaongezea uelewa na kuwajenga ujasiri katika kukipigania chama cha mapinduzi na kukiwezesha kuweza kushinda awamu kwa awamu.
Wamesema mafunzo hayo yamekuja wakati muwafaka ambayo yametoa fursa kwa wajumbe kujadili na kujifunza mambo mbali mbali yaliyomo ndani ya chama ikiwemo utunzaji wa siri, sambamba na kujipanga juu ya kufikia malengo ya chama cha mapinduzi.
Imetolewa na Kitengo cha Habari ( OMPR )
.jpeg)
0 Comments