Kamisheni ya Kukabiliana na maafa Zanzibar imeitaka Jamii kujiepusha na vitendo hatarishi vinavyopelekea kusababisha athari za majanga hasa katika kipindi hicho cha mvua zinazoendelea kunyesha.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Utawala, Mipango na Rasilimali watu kutoka Kamisheni ya Kukabiliana na Maafa Zanzibar Haji Ame Haji wakati akifungua Mafunzo kwa Wajumbe wa Sheha katoka Katika Shehia ya Muembe Makumbi na Karakana huko Skuli ya Muembe Makumbi.,Wilaya ya Mjini .
Amesema kuwa katika kipindi cha mvua hujitokeza adhali mbali mbali za majanga ya Maafa ambazo baadhi husababishwa na Jamii ikiwemo.janga la maradhi ya mripuko pamoja na mafuriko hivyo ni vyema Jamii kuweka hali ya usafi wa mazingira yao ili kujiepusha na janga hilo
Akitoa elimu kwa Wajumbe wa Sheha Afisa Afya Wilaya Nasriya Mohammed amesema ugonjwa wa mripuko huwaadhiri watu wengi Kwa muda mchache jambo ambalo linachangia kusababisha vifo na kupotesa nguvu kazi ya Taifa .
Amefahamisha kwamba Mazingira yakiwa machafu yanapelekea kuzuka maradhi ya mripuko sambamba na muimgiliano ya watu huchangia kuenea maradhi ya kuambukiza .
Amesema Kumekuwa na tabia ya Baadhi ya watu kutupa taka Katika miundombinu ya mitaro ya maji ya mvua jambo ambalo husababishwa kuziba na kupelekea kufurika Kwa maji ya mvua majumbani .
Amefahamisha kwamba Jamii ichukuwe tafadhali za mapema Katika kuwekwa Mazingira yao katika hali ya usafi ili kuweza kudhibiti janga hillo hasa katika kipindi hicho cha mvua .
Nae Mkaguzi kutoka Kituo cha Zimamoto na Uokozi, Idrisa Khamis Mwinyi, amewaasa wajumbe hao kuachana na mazoea ya kuacha vifaa vya umeme vikiwa wazi wakati wamelala, kwani hali hiyo inaweza kusababisha hitilafu ya umeme (short circuit) na kupelekea majanga ya moto.
Amesema jamii inapaswa kuelewa kuwa kuchaji simu usiku bila uangalizi, pamoja na kuacha vifaa vya umeme vikiwa vimewashwa, ni hatari kubwa iwapo kutatokea hitilafu ya umeme.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa jamii kuweka utaratibu mzuri wa matumizi ya majiko ya kupikia ili kuepusha ajali na majanga ya moto majumbani.
Kwa upande wake, Sheha wa Shehia ya Karakana, Juma Othman Abdalla, amewataka wajumbe hao kuitumia elimu waliyoipata kuwa mabalozi wazuri kwa jamii, kwa lengo la kutoa uelewa kuhusu athari za maradhi ya mlipuko na umuhimu wa kudumisha mazingira safi.
By Khadija Khamis
WHSUM

0 Comments